WAELEWE MATAPELI WALIOKUBUHU HAPA DSM....IMENITOKEA MM LEO 02/02/2013 KWA
MARA YA PILI
Kuna utapeli fulani unaendelea Tanzania na inaelekea wanaoufanya wamefanikiwa
sana na wanaendelea kufanikiwa kwani ni wa muda mrefu sasa. Nadhani matapeli
hawa wanatumia ujinga wetu maana sisi sio watu wakutafuta sana usahihi wa mambo
kabla ya kusema au kutoa maamuzi, pamoja na ujinga wetu wa kutaka kufanikiwa kwa
haraka kwa njia yeyote ile hata kama hatujafanya kazi na bila kutumia akili. Utapeli huu
sio mwingine bali ni ule wa wale watu wanaompigia mtu simu wakijifanya wanakujua
kabisa na wanaweza hata kukupa some backgrounds zako za kazi, ajira au elimu
na meninge hadi ukashawishika kuwa unayeongea naye ni mtu unayemfahamu/
munayefahamiana na hivyo kutokua na hofu na uhalisia wa anachokuambia. Baada ya
hapo wanaanza kukushawishi juu ya kuwasaidia kupata madawa ya kuhifadhi nafaka
kwa madai kuwa mawakala wao ambo wamekua wakizipata toka kwao wameanza
kuleta uswahili hivyo kwa vile unayeongea naye ndio anahusika na suppy, basi ameona
ni vema akutumie wewe “mpendwa anayekujua” ili angalau upate hiyo commission
kubwa ambayo huwapa ho mawakala na mugawane kidogo. Mara nyingi wanasema
wanafanya kazi na shirika la chakula duniani (FAO) au shirika la wakimbizi duniani
(UNHCR) na wako Kigoma.
Zaidi ya mwaka mmoja sasa nikiwa ofisini walinipigia na aliyekua anaongea name
alianza kwa kujitambulisha kama graduate wa kitivo cha uhandishi cha chuo Kikuu
Mlimani na kwamba tulisoma wote mwaka mmoja wakati nikisoma degree ya kwanza
lakini huenda simkumbuki kwa sababu nilikua kiongozi wa fellowship na siwezi kuwa
nakumbuka wote niliokua nawaongoza. Yeye alikua fellowship. Alikua akiongea kwa
kicheko na “bwana yesu” asifiwe nyingi ili kunionesha ni kwa kiasi gani namfahamu
na tunafahamiana. Kwa bahati mbaya wakati ananipigia nilishasikia kwa umbali juu
ya utapeli huo ambao kwa kipindi hicho ndio ulikua umeanza tu na kushika kasi huku
watu wengi wakiwa wamepoteza mamilioni. Hivyo alipoanza kuongea ujinga wake wa
kunipa commission and all that, nilimwambia tu kuwa sina muda wa kujihusisha na
biashara aliyokua “anataka kunisaidia ili nipate pesa za bure”, kwa haraka na bila jasho.
Alikua disappointed sana kwa jibu langu hasa kutokana na muda mrefu alioutumia
kunishawishi nikubali “msaada aliokua ananipa kama mpendwa mwenzake”.
Leo asubuhi majira ya saa nne nilipokea simu kwenye line yangu ya tigo na number
iliyonigia ni 0717-093260. Mtu aliyenipigia alikua anaongea kwa uchangamfu mkubwa
na kwa furaha huku akitaja majina yangu yote na kuniuliza iwapo kwa sasa niko DSM
au nimesafiri. Aliniambia kuwa kafurahi kusikia kuwa niko DSM kwani ndipo zilipo ofisi
zao na kwamba alitaka kuniunganisha zao ili nikachukue mzigo ambao utakua na cha
juu kizuri sana. Nilipoona anaendelea nilimuomba ajitambulishe...akaniambia anaitwa
Lameck na kuwa alishafanya kazi Planet International hapa chuo kikuu. Alipotamka
hivyo nikaanza kupata ukakasi kwani hapajawahi kuwa ofisi ya kampuni hiyo hapa
Mlimani. Nikamuuliza yuko wapi kwa sasa na kwa msisitizo akanijibu kuwa kwa sasa
yuko Serengeti National Park. Nikamuuliza iwapo anafanya kazi na TANAPA..akasema
hapana bali yuko na shirika moja la Kijerumani linalojishughulisha na wanyamapori...na
akijua kuwa niko Chuo Kikuu alitafuta style nzuri ya “kuniingiza alipokusudia” ...maana
alianza kunieleza kuwa shirika lao linafanya “tafiti za wanyama pori katika mbuga
yetu ya Taifa kubwa sana”. Bado nikiwa najaribu kuunganisha “idadi ya nukta kadhaa”
akaniona mjinga sana na kuanza kunielezea jinsi wanyawa walioko Serengeti wanavyo
migrate kila mwaka kwenda Kenya.....na kuwa wanahama wengi kama elfu mbili
hivi...(nikapata nukta nyingine)..then nikaingilia na kumsaidia kuwa hawavuki kwa
maelefu bali ni zaidi ya milioni moja wanahama na kurudi kila mwaka. Pomaja na utafiti
kazi nyingine wanayofanya ni pamoja na kutoa chanjo kwa wanyama hawa maana
wanaporudi wanakua wamerudi na magonjwa toka Kenya.
Hapa ndipo alipopotea njia zaidi kwani kati ya jambo ninalolijua kwa mapana
kidogo ni hii movement ya wild beasts, zebra na wengine walioko Serengeti .
Nikamuonesha kushangaa kuwa wanawezaje kuwapa chanjo
namna hii (na kumuonesha najua chanjo ni nini nikajifanya mhaya kidogo na kutamka
vaccination)...akaanza kujichanganya kuwa wao wana njia tatu za kutoa chanjo
maana ni kweli kuwa wanyama ni wengi...kwanza wanatengeneza majosho/mabwawa/
madimbwi ambayo wanaweka dawa na hiyo wale wanyama wanapokua wanarudi
wanatumbukia na hivyo automatically wanakua wamepata chanjo. Hapa akachemka
zaidi...nikamuuliza hivi kuogesha ng’ombe kwenye majosho ni chanjo au ni kuua
kupe na viroboto? Nikamuuliza kuna chanjo inafanyika juu ya ngozi?...alipoona hana
majibu akauma maneno mawili-matatu halafu akasema njia ya pili wanayotumia
ni kuwakamata wale wakubwa kama tembo na wengine na kuwapiga sindano za
chanjo....nikajizuia kucheka. Alipoona swali lingine linafuata kabla hajaanza kuningiza
kwenye “undani/details za deal” lenye commission ...akaomba udhuru kidogo kuwa
boss wao kaingia ofisini mara moja na hivyo atanipigia baadaye kidogo...akakata simu
na ukawa ndio mwisho wa mawasiliano
Alipokata simu tu nikamtext kuwa angeendelea tu na ujinga wake maana nawafahamu
vema na wanachokifanya...na huo ukawa ndio mwisho wa ile number kupatikana
hewani baada tu ya ujumbe wangu kuwa delivered.
Ushauri Kidogo:
• Unapojikuta kwenye mazingira ya mtu kujitambulisha kwako kwa nguvu kubwa huku
ukiwa humfahamu, mpe nafasi ya kuongea
• Unapojikuta kwenye mazingira ya kudanganyika kuwa unaweza kunufaika na kupa
utajiri kirahisi kwa mtindo wa ki_DECI_DECI au kimuujizaujiza, usichanganyikiwe
na kuanza kuutazama huo muujiza kama ndio umeshakufikia. Utafanya la muhimu
sana iwapo utaruhusu akili yako kufanya kazi na kutafakari vema kila unachokiona
au kukisikia
wanyama wengi
Kama unaweza, ni vema kurecord mazungumzo ambayo una wasiwasi nayo
• Kama unaweza, una nafasi, na una matumaini kuwa polisi wanaweza kuwa na
msaada kwenye hili, basi wasikilize watu hawa na kutafuta msaada wa polisi kwani
utaokoa na wengine wasidanganyike
• Tambua tu kuwa watu hawa wana mtandao mkubwa sana na mara nyingi
wanafanya mambo yao wakiwa na taarifa za kuwatosha na wamejipanga. Unaweza
ukawa kwenye mstari mwembamba sana unaotofautisha ukweli na uongo
• Kwa nini bado makampuni ya simu yanaruhusu simu kutumika ikiwa haijasajiliwa?
Na kama imesajiliwa, je wale wanaoandikisha hizi simu, wana ujuzi wowote wa
kugundua kitambulisho halali na ambacho ni fake watu wanavyovitumia kusajilia
simu zao?
Ufahamu na Akili tuliyonayo ukitumika vema bil haraka ya mafanikio tunaweza kukabiliana
na changamoto nyingi za kitapeli tunazokumbana nazo
IMEANDIKWA NA
MATHEW MNDEME a.k.a MM
No comments:
Post a Comment